93.0 Mambojambo FM - Arusha, Tanzania

  • MTAA WA PILI
    BUGARABU
    LATE DATE
    NIGHT EXPRESS
    DANCEHALL
    REGGAE NYT FEVER
    KWETU AFRICA
    FLASHBACK
    JOY TO THE WORLD
    MAZINGIRA
    MAISHA
    SMOOTH SUNDAY

 

MAMBO JAMBO RADIO ONLINE


NEWS

KIGODA AMG'OA CHARLES EKELEGE

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda asema Mkurugenzi wake Mkuu, Charles Ekelege anatakiwa kusimamishwa kazi ili kupisha taratibu za kisheria ikiwamo suala la uchunguzi dhidi yake kufanyika hivyo ameiagiza Bodi ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kumsimamisha kazi.
“Moja ya sababu iliyomfanya Rais afanye mabadiliko ya uongozi katika wizara hii ni Shirika la TBS. Kulikuwa na mjadala mkubwa bungeni kuhusu utendaji wake. Nimewataka bodi ya shirika hilo kumsimamisha kazi mkurugenzi huyo mara moja ili kupisha utaratibu mwingine wa kisheria kuanza.”
Dk Kigoda ametoa kauli hiyo ikiwa ni mara ya kwanza kuzungumza na waandishi wa habari tangu kuteuliwa kwake na Rais Jakaya Kikwete kushika wadhifa huo baada ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri hivi karibuni.
Wakati akitangaza Baraza hilo, Rais Kikwete alizungumzia azma ya Serikali kuchukua hatua kwa watendaji wengine wa Serikali na taasisi zake ambao alisema ni chanzo cha mabadiliko hayo.
Rais Kikwete alisema mawaziri wamekuwa wakijiuzulu hata kwa makosa ambayo si yao na kwamba Serikali itaanza kuchukua hatua kwa watendaji wakiwamo makatibu wakuu, wakurugenzi wa wizara, watendaji wakuu wa mashirika na taasisi za umma pamoja na bodi za mashirika husika.
“Pamoja na kuwa na utaratibu huu mzuri wa kuwajibika kwa wanasiasa, sasa lazima tuwawajibishe hata hao wanaosababisha mawaziri hawa kujiuzulu, maana wakati mwingine wanawajibika kwa makosa ambayo si yao,” alisema Kikwete.

RIBA NAFUU KWA WAKULIMA NCHINIWaziri Mkuu, Mizengo Pinda amezitaka benki nchini kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa wakulima  ili waweze kuendelea kilimo.Pinda alisema hayo jana jijini Dar es Salaam katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Chama cha Kilimo Vijijini Afrika (Afraca).Katika hotuba hiyo Pinda alisema kwamba, ni muhimu benki hizo zikafika vijijini ili wakulima hao waweze kupata fedha za kuendelezakilimo chao.
"Wakulima wadogowadogo wanashindwa kupata mikopo ya kutosha kwa sababu benki za biashara zinawatoza riba kubwa na kuhitaji dhamana,"alisema Pinda.
Alisema kutokana na hali hiyo, wakulima hao wamekuwa wakishindwa kupata mikopo kwa kuwa wanaonekana hawawezi kulipa.
"Kutokana na hali hii, taasisi za fedha zijenge uhusiano wa karibu na vyama vya kuweka na kukopa ili kupunguza kukoseka kwa mikopo hasa maeneo ambayo benki hazijafika,"alisema.
Alisema ni matumaini yake kuwa mkutano huo utaangalia jinsi ya kutatua changamoto hiyo ya upatikanaji wa fedha ili sekta ya kilimo iweze kukua.

POLISI 700,JWTZ 248 WAUMBUKAMamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), imebaini kuwa Jeshi la Polisi lina askari 700 wenye majina yanayofanana na waajiriwa wengine serikalini huku Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) likiwa na askari 248.
Mkurugenzi Mkuu wa Nida, Dickson Maimu alisema jana Dar es Salaam kwamba watumishi hao wamebainika kutumia cheti kimoja cha elimu na mtu mwingine jambo ambalo lilikuwa changamoto kubwa wakati ilipoanza uandikishaji kwa watumishi wa Serikali.
Maimu alikuwa akitoa kwa waandishi wa habari, taarifa ya utekelezaji wa mradi wa vitambulisho vya Taifa na kubainisha kuwa hiyo ni dalili kwamba watumishi wake watakabiliwa na changamoto kubwa katika kuhakikisha kwamba kila Mtanzania anapata kitambulisho cha uhakika.
“Kwa hivi sasa maeneo tuliyopitia tumegundua kuna utumiwaji wa vyeti mara mbili vyenye jina moja na mkitaka niwatajie. JWTZ tumekuta watu 248 na Polisi watu 700 ambao vyeti vyao vinatumiwa na watu wawili tofauti,” alisema Maimu.
Kuhusu hali ya mradi, Maimu alisema wameamua kisitisha kwa muda uzinduzi wa vitambulisho hadi Juni Mosi, mwaka huu siku ambayo vitambulisho hivyo vitaanza kutolewa kwa wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam.
“Mamlaka ya vitambulisho vya taifa imekamilisha hatua zote na tuko tayari kuzindua mradi wetu na kutoa vitambulisho. Ha ta hivyo, zimejitokeza changamoto na mahitaji ya msingi kutoka kwa wadau wetu muhimu ambavyo hatuna budi kuvifanyia kazi kwanza ili kitambulisho kiwe kimekidhi mahitaji yote
MIRIAM ODEMBA AMTESA KARDASHIANWanawake wazuri kama Kim Kardashian nao huwa wanateswa na wivu Inasemekana Odemba aliwahi kukutana na Kanye West na kujuana mwaka jana wakati rapa huyo akizindua nguo za kwanza huko Ufaransa.
Sasa wikiendi hii Kanye West alipokwenda tena Odemba baada ya kumuona rafiki yake, alimchangamkia na kujumuika naye kucheza muziki kitendo ambacho hakikumfurahisha Kim amini usiamini Miriam Odemba alimnyima raha mlimbwende huyo baada ya kuwa bega kwa bega na 'boy frend' wake, Kanye West.
Inadaiwa kuwa Kim alianzisha patashika nyuma ya jukwaa wakati mpenzi wake huyo akizindua nguo zake mpya huko Ufaransa.
Kim na Kanye walikuwa Paris kwa shughuli hiyo na Odemba yuko huko Ufaransa kwa kazi yake ya kuonyesha mavazi.
Wakati Kanye akicheza na Odemba, Kim alikuwa amekaa na Swizz Beatz na mkewe Alicia Keys, unaambiwa Kim alikuwa hapepesi macho kwa wivu.
Hata hivyo Kim anadaiwa kuwa alishindwa kuendelea kuvumilia kuona mwanamke mrembo akiendelea kucheza na mpenzi wake na kuhatarisha penzi lao changa. Moja kwa moja alimvuta Kanye huku maneno yakimtoka.
Mastaa wengine waliohudhuria shughuli hiyo ni pamoja na
  D’Banj, P.Diddy, common, Big Sean, Cassie na Waka Flocka Flame.